PaPi Clever & Dorcas - Kitambo Bado Lyrics

Contents:

Kitambo Bado Lyrics

Kitambo bado-vita itaisha, kitambo, na dhoruba zitapoa
Na tena nitalaza kichwa changu mbavuni mwake anayenipenda
Kitambo bado-vita itaisha, kitambo, na dhoruba zitapoa
Na tena nitalaza kichwa changu mbavuni mwake anayenipenda
Nitaziona raha na amani, mbinguni hazitakuwapo dhambi
Nitaziona raha na amani, mbinguni hazitakuwapo dhambi

Kitambo bado- roho yaumizwa, kitambo katika usiku huku
Machozi nina’toka mara nyingi sababu sijaona bado Yesu
Kitambo bado- roho yaumizwa, kitambo katika usiku huku
Machozi nina’toka mara nyingi sababu sijaona bado Yesu
Lakini asubuhi ya milele huko mbinguni sitalia tena
Lakini asubuhi ya milele huko mbinguni sitalia tena

Kitambo bado ya kuchoka huku, kitambo, tena nitaona Yesu
Na huru mbali na hatari zote nitastarehe mikononi mwake
Kitambo bado ya kuchoka huku, kitambo, tena nitaona Yesu
Na huru mbali na hatari zote nitastarehe mikononi mwake
Uvuli wote utaondolewa kwa nuru huko kamilifu kweli
Uvuli wote utaondolewa kwa nuru huko kamilifu kweli

Mateso yangu hayadhuru tena, nitasahau yote kwa Yesu
Nikisumbuka mda duniani, mbinguni sitaona shida, kufa
Mateso yangu hayadhuru tena, nitasahau yote kwa Yesu
Nikisumbuka mda duniani, mbinguni sitaona shida, kufa
Na Mungu atafuta kila chozi, ataondoa maumivu yote
Na Mungu atafuta kila chozi, ataondoa maumivu yote


PaPi Clever & Dorcas Songs

Related Songs